Ijumaa, 13 Januari 2017

SELINE AFUNGUKA KWA WA SANII WAKIKE KUTUMIA SKENDO KUJIPATIA UMAARUFU

Msanii wa kike  ambae aliyewahi kuwa chini ya label ya The Industry iliyo chini ya kundi la Navy Kenzo linaloundwa na wasanii Aika na Nahreel, Seline amefunguka  sana kuhusiana na wasanii wa kike kutumia skendo kwa kujiongezea umaarufu.



Akizungumza na Mtangazaji Pk5tz wa kipindi cha Extra Fleva cha Uplands FM ya Njombe, Seline ambaye sasa yupo chini ya usimamizi wa Producer Mona Gangstar wa Classic Sound, amesema kitu anachokichukia kwa sasa ni wasanii wa kike kutumia skendo kwa ajili ya kupromote kazi zao.


Seline amedai wakati mwingine ni nzuri sababu zinamfanya msanii azungumziwe ingawa wakati mwingine ni vyema msanii akaamini katika kipaji alichonacho kwakuwa skendo zina changamoto yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni